MBUNGE WA MOSHI MJINI MZEE PHILEMON NDESAMBURO AMTANGAZA MRITHI WAKE


Hatimaye Mbunge wa Moshi Mjini mzee Philemon Ndesamburo amemtanga rasmi Meya wa manispaa ya Moshi Ndg Michael Japhari kuwa mrithi wa kiti chake cha Ubunge wa Moshi Mjini 2015.
Meya Japhari ni Diwani wa kata ya Bomambuzi ambaye ameiongoza manispaa ya Moshi kwa uadilifu na mafanikio makubwa.
Meya Japhari pia ni Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Moshi Mjini ambapo amefanikiwa kuwaongoza wana Chadema wa Moshi Mjini kushinda mitaa 31 dhidi ya 29 ya CCM na hatimae kuifanya Chadema kuwa chama tawala Moshi Mjini.
Chadema wa Moshi Mjini wanampenda na kumheshimu sana Mzee Ndesa hivyo watabariki uamuzi wake wa kumpendekeza Meya Japhary kuwa mrithi wake na hivyo nina hakika Chadema wa Moshi Mjini watampitisha kwa kishindo Meya Japhary kwenye kura za maoni ndani ya chama kwa mujibu wa katiba.

No comments: