MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI MH JOSHUA NASSARI AMEPOKEA NYUMBA MBILI ZA KISASA KUTOKA KWA WAFADHILI

Mh Joshua Nassari alipokutana na wafadhili kutoka Switzelanda kwaajili ya makabidhiano ya nyumba za Waalimu katika Shule ya Sekondari Momella
Mhe Mbunge wa arumeru Mashariki amepokea rasmi wa nyumba za kisasa za walimu (two in one), shule ya sekondari momella - kata ya ngarenayuki.

Huu ni msaada toka switzeland. Mhe Mbunge aliambatana na katibu na mkiti wa chadema Wilaya , madiwani wa ngabobo, Uwiro na mwenyekiti wa kijiji cha Olkung'wado mzee Malimwengu (CDM) ambaye pia amekuwa msimamizi mkuu wa mradi huu.

Mhe Nassari pia aliwakaribisha wahisani hawa nyumbani Kwake Kwa Chakula cha mchana ambapo walikubaliana kuendeleza ushirikiano.
"Nimeshiriki kazi za maendeleo MERU tangu mwaka 1994 lakini hakuna Mbunge hata mmoja aliyewahi kujali au kukutana na sisi, wewe ni wa kwanza kufanya hivyo" alisema Emily Karafiat, mwakikishi wa wahisani.





No comments: