TAARIFA KUHUSU MAAZIMIO YA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHADEMA


Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari na umma kuwa, baada ya siku 4 za kikao cha dharura cha Kamati Kuu, kesho chama kupitia mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika Jumatano, Julai 27, 2016, ukihusisha waandishi waandamizi na wahariri wa vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa, chama kitatangaza maazimio ya kikao hicho kilichohitimisha vikao hivyo leo Jumanne, jijini Dar es Salaam.
Awali, kikao hicho cha dharura kilipangwa kufanyika kwa siku 2 lakini kutokana na umuhimu na uzito wa masuala yaliyojadiliwa kikao kililazimika kuendelea kwa siku zingine mbili za ziada, ambapo Kamati Kuu ilipokea taarifa ya kina juu ya masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na hali ya siasa nchini kwa sasa ambayo inatishia hali ya uchumi na ustawi wa jamii nzima kwa ujumla, hivyo taifa zima kuwa katika majaribu makubwa ya kukosa mwelekeo wa kiuongozi.
Kupitia mkutano huo, chama kitazungumzia mipango ya kujiimarisha kuendelea kuwatumikia wananchi na kusimamia dira ya MABADILIKO ya kweli na UHURU wa kweli nchini.
Aidha, chama kupitia mkutano huo, kitatoa mwelekeo wa hali ya nchi hasa wakati huu ambapo taifa linaonekana kukosa dira ya uongozi kwa ajili ya ustawi wa Watanzania wote kwa ujumla.
Imetolewa leo Jumanne, Julai 26, 2016 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

1 comment:

ieeshiaihlenfeldt said...

MGM National Harbor is now live with a new $10,000
MGM National Harbor 익산 출장마사지 is now live 군포 출장안마 with a new $10,000,000 경산 출장안마 renovation,” said Steve B. Johnson, president of 태백 출장마사지 the casino and 목포 출장샵 entertainment